Kampuni ya Agreen Mind Limited ni kampuni binafsi yenye ukomo kupitia Hisa. Kampuni hii imesajiliwa chini ya Sheria ya makampuni kupitia Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) nchini Tanzania, na kutunukiwa cheti cha usajili namba
152801440
Dhamira Yetu
Kuwekeza katika kilimo na kuzingatia matumizi bora ya rasilimali kwa malengo ya kuleta maisha bora kwa jamii inayotuzunguka.
Maono Yetu
Jamii endelevu yenye uchumi unaostawi.
Shughuli tunazofanya
Kilimo- Biashara
Elimu ya Ukombozi Wa Kifikra.
Viwanda na Masoko
SHUGHULI ZINAFANYIKA MKOANI IRINGA WILAYA YA KILOLO
Parachichi ni zao linalooteshwa katika ukanda wa baridi na katika ardhi yenye rotuba na maji ya kutosha. Iringa, Arusha, Mbeya, Morogoro, Njombe, Tanga na Kilimanjaro ni baadhi tu ya mikoa inayolima Parachichi kwa wingi hapa Tanzania.
Kampuni ya Agreen Mind Limited tumechagua kulima Parachichi katika mkoa wa Iringa,Wilaya ya Kilolo.